sw_tw/bible/other/refuge.md

12 lines
728 B
Markdown

# Kimbilio, malazi
## Ufafanuzi
"Kimbilio" ni sehemu au hali ya usalama na ulinzi. "Malazi" ni sehemu yenye muundo wa kimwili ambayo inakulinda kutokana na hali ya hewa au hatari.
* Katika Biblia Mungu anaelezwa kama kimbilio ambapo watu wake huwa salama na kupata ulinzi kwake.
* "Mji wa makimbilio" katika agano la kale ni miji ambayo mtu akiua kwa bahati mbaya hukimbilia huko kwa ajili ya usalama toka kwa watu wanaotaka kumvamia na kulipa kisasi.
* Malazi ni sehemu inayojengwa kama jengo ambalo laweza kutoa ulinzi kwa watu au wanyama.
* Mara nyinginge malazi humaanisha usalama. Lutu aliposema wageni wake wapo chini ya malazi ya paa lake alikuwa na maana kuwa walikuwa salama kwa sababu walikuwa kwenye nyumba yake.