sw_tw/bible/other/lion.md

572 B

simba

Ufafanuzi

Simba ni mnyama mkubwa wa porini anayefanana na paka, mwenye meno yenye nguvu na makucha ya kuulia na kurarua mawindo yake.

Simba wana miili yenye nguvu na kasi kubwa ya kushika mawindo yao. Manyoya yao ni mafupi na yana rangi ya mchanganyiko wa kahawa na dhahabu. Simba dume wana manyoya ya shingoni yanayozunguka vichwa vyao. Simba huua wanyama wengine ili kuwala na pia wanaweza kuwa hatari kwa binadamu. Mfalme Daudi alipokuwa mvulana, aliua simba waliojaribu kuvamia kondoo wake aliokuwa akiwachunga. Samsoni pia aliua simba kwa mikono yake.