sw_tw/bible/other/king.md

995 B

mfalme

Ufafanuzi

Neno "mfalme" linamaanisha mwanamme ambaye ni mtawala mkuu wa mji, jimbo, au nchi.

Mfalme kawaida huchaguliwa kutawala kwa sababu ya uhsiano wake kifamilia na wafalme wa nyuma. Mfalme anapokufa, kawaida mwana wake mkubwa ndiye anayekuwa mfalme mpya. Katika nyakati za zamani, mfalme alikuwa na mamlaka yote juu ya watu katika ufalme wake. Neno "mfalme" halitumiki sana kwa mtu asiye mfalme wa kweli, kama "mfalme Herode" katika Agano Jipya. Katika Biblia, Mungu anajulikana kama mfalme anaye tawala juu ya watu wake. "Ufalme wa Mungu" unamaanisha utawala wa Mungu juu ya watu wake. Yesu aliitwa "Mfalme wa Wayahudi," "mfalme wa Israeli," na "mfalme wa wafalme." Yesu atakaporudi, atatawala kama mfalme wa dunia. Neno hili linaweza kutafsiriwa kama, "mkuu" au "kiongozi kamili" au "mtawala mwenye nguvu." Usemi "mfalme wa wafalme" unaweza kutasiriwa kama "mfalme anayetawala juu ya wafalme wengine wote" au "kiongozi mkuu aliye na mamlaka juu ya viongozi wengine wote."