sw_tw/bible/other/integrity.md

457 B

uadilifu

Ufafanuzi

Neno "uadilifu" inamaanisha kuwa mwaminifu, na mwenye msimamo mkali wa maadili na tabia.

Kuwa na uadilifu ni kuchagua kutenda kilicho kweli na sawa hata wakati hakuna mwingine anayetazama. Baadhi ya watu katika Biblia, kama Yusufu na Danieli, walionesha uadilifu walipokataa kufanya uovu na kuchagua kumtii Mungu. Kitabu cha Mithali kinasema kuwa ni bora kuwa maskini na kuwa na uadilifu kuliko kuwa tajiri na mfisadi na muongo.