sw_tw/bible/other/house.md

1.0 KiB

Nyumba

Ufafanuzi

Istilahi 'nyumba' hutumika kama tamathali ya semi (mfano) katika Biblia. Mara nyingine hutumika kumaanisha 'kaya' kurejelea watu wanaoishi pamoja katika nyumba. Mara zote neno 'nyumba' humaanisha wazao au watoto au ndugu wengine. Mfano, nyumba ya Daudi huwa na maana ya uzao wa Daudi. Maneno kama 'nyumba ya Mungu' au 'nyumba ya Yahweh' huwa na maana ya hekalu au hema la kukutania au sehemu Mungu alipo. Katika Waebrania 3, "Nyumba ya Mungu" ni sitiari ikimaanisha Watu wa Mungu. Kifungu cha maneno ' nyumba ya Israeli" kwa ujumla huwa na maana ya taifa laote la Israeli au hasa hasa kwa makabila ya ufalme wa Kasikazini wa Israeli.

Mapendekezo ya tafsiri kwa kutegemeana na muktadha, neno, nyumba linaweza kuwa na maana ya 'kaya' ' watu, familia, uzao, hekalu au sehemu ya kukaa.'' "Nyumba ya Daudi' in maana ya ''ukoo wa Daudi, familia ya Daudi au uzao wa Daudi. "Nyumba ya Israeli' ina maana ya watu wa Israeli au wazao wa Israeli au waisraeli. 'Nyumba ya Yahweh' ina maana ya hekalu au sehemu ya kumwabudia Mungu.