sw_tw/bible/other/hand.md

1.7 KiB

mkono, mkono wa kuume,

Ufafanuzi

Neno 'mkono' limetumika katika Biblia kama lugha ya picha kwa njia mbalimbali Kuweka kitu katika mikono ya mtu fulani inamaana ya kukabidhi kitu hicho. Neno 'mkono' limetumika kurejelea uweza au nguvu ya Mungu na matendo yake. kwa mfano, Mungu anaposema "je si mkono wangu uliyoyafanya haya?" Neno "kabidhi" hurejelea maana ya kuweka kitu katika mkono au utawala wa mtu fulani. Kuweka mikono juu ya mtu fulani mara nyingi huambatana na utoaji wa baraka kwa mtu huyo. Pia kitendo cha 'kuweka mikono" juu ya mtu kinamaanisha kumweka mtu huyo wakfu kwa ajili ya kazi ya Mungu au kwa ajili ya kumwombea mtu huyo uponyaji. Baadhi ya lugha za picha za neno mkono ni: Kunyosha mkono juu ya mtu maana yake ni kumdhuru. ''kumwokoa kutoka katika mkono wa..." ni kumzuia mtu ili asimdhuru mtu mwingine. matumizi mengine ya mkono ni kama: "kunyosha mkono" ina maana ya 'kudhuru' au kuumiza" "kumwokoa mtu mikononi mwa" ina maana ya kumzuia mtu ili asimdhuru mtu mwingine. "kuwa karibu na mkono " kuwa 'karibu' "kuwa mkono wa kuume" humaanisha kuwa 'nafasi'' au ''sehemu ya'' au "upande wa kulia" Maelezo yanayosema "kwa mkono wa'' au ''kupitia mkono'' ina maana kuwa kitendo kimefanya na mtu huyo. kwa mfano, "kwa mkono wa Bwana'' ina maana kuwa Bwana ndiye amefanya tendo hilo. Wakati Paulo anasema " imeandikwa kwa mkono wangu" ina maana kuwa sehemu hii ya barua iliandikwa kwa mkono wake kabisa, badala tu kusema na mtu mwingine akayaandika.

Mapendekezo ya tafsiri. Maelezo haya na tamathali hizi za semi zaweza kutafsiriwa kwa kutumia lugha zingine za picha ambazo zina maana sawa. Au maana inaweza kutafsiriwa kwa kutumia lugha ya moja kwa moja.