sw_tw/bible/other/forever.md

945 B

milele

Ufafanuzi

Katika Biblia, msemo "milele" una maana ya muda usiofika mwisho. Mara kwa mara hutumika kitamathali kumaanisha, "muda mrefu sana".

Msemo "milele na milele" unasisitiza ya kwamba jambo litakuwepo milele.

Msemo "milele na milele" ni njia ya kuelezea maisha ya milele yakoje. Pia una wazo la muda ambao hauishi.

Mungu alisema ya kwamba ufalme wa Daudi utakuwepo "milele". Hii inamaanisha ukweli ya kwamba uzao wa Daudi Yesu atatawala kama mfalme milele.

Mapendekezo ya Tafsiri

Msemo huu unaweza kutafsiriwa kama "mara zote" au "kutokuwa na mwisho". Msemo, "utadumu milele" unaweza kutafsiriwa kama "kuwepo mara zote" au "hautakoma" au "utaendelea mara zote". Msemo wa kishindo, "milele na milele" unaweza kutafsiriwa kama "kwa mara zote na zote" au "kutomalizika" au "ambayo haifiki mwisho". Ufalme wa Daudi kudumu milele unaweza kutafsiriwa kama, "uzao wa Daudi atatawala milele" au "uzao wangu ataendelea kutawala".