sw_tw/bible/other/fire.md

570 B

moto

Ufafanuzi

Moto ni joto, mwanga na miale ambayo hutokana pale kitu kinapochomwa.

Kuchoma mbao kwa moto hugeuza mbao kuwa majivu.

Msemo "moto" pia hutumika kitamathali, mara kwa mara kumaanisha hukumu au utakaso.

Hukumu ya mwisho ya wasioamini ipo katika moto wa jehanamu.

Moto hutumika kusafisha dhahabu na vyuma vingine. Katika Biblia, hatua hii hutumika kuelezea jinsi Mungu husafisha watu kupitia mambo magumu ambayo hutokea katika maisha yao.

Msemo "kuwabatiza kwa moto" unaweza kutafsiriwa kama "kukusababisha upitie mateso ili kwamba yakusafishe"