23 lines
788 B
Markdown
23 lines
788 B
Markdown
# sikukuu
|
|
|
|
## Ufafanuzi
|
|
|
|
Kwa ujumla, sikukuu ni sherehe iliyofanyika na jamii ya watu.
|
|
|
|
Neno kwa ajili ya "sikukuu" katika Agano la Kale lina maana ya "muda ulioteuliwa".
|
|
|
|
Sikukuu zinazosherehekewa na Waisraeli zilikuwa nyakati maalumu zilizoteuliwa au nyakati ambazo Mungu aliwaamuru wao kuzifuata.
|
|
|
|
Katika baadhi ya tafasiri za Kiingereza, neno "sikukuu" linatumika badala ya karamu kwa sababu sherehe zilijumuisha mlo mkubwa wa pamoja.
|
|
|
|
Kulikuwa na karamu kadhaa ambazo Waisraeli walisherehekea kila mwaka:
|
|
Pasaka
|
|
Sikukuu ya Mkate Usiotiwa Chachu
|
|
Mavuno ya Kwanza
|
|
Sikukuu ya Wiki (Pentakuki)
|
|
Sikukuu ya Tarumbeta
|
|
Sikukuu ya Kulipia Kosa
|
|
Sikukuu ya Vibanda
|
|
Kusudi la sikukuu hizi ilikuwa kumshukuru Mungu na kukumbuka mambo ya ajabu aliyofanya kuwaokoa, kuwalinda na kuwapa watu wake.
|
|
|