sw_tw/bible/other/festival.md

788 B

sikukuu

Ufafanuzi

Kwa ujumla, sikukuu ni sherehe iliyofanyika na jamii ya watu.

Neno kwa ajili ya "sikukuu" katika Agano la Kale lina maana ya "muda ulioteuliwa".

Sikukuu zinazosherehekewa na Waisraeli zilikuwa nyakati maalumu zilizoteuliwa au nyakati ambazo Mungu aliwaamuru wao kuzifuata.

Katika baadhi ya tafasiri za Kiingereza, neno "sikukuu" linatumika badala ya karamu kwa sababu sherehe zilijumuisha mlo mkubwa wa pamoja.

Kulikuwa na karamu kadhaa ambazo Waisraeli walisherehekea kila mwaka: Pasaka Sikukuu ya Mkate Usiotiwa Chachu Mavuno ya Kwanza Sikukuu ya Wiki (Pentakuki) Sikukuu ya Tarumbeta Sikukuu ya Kulipia Kosa Sikukuu ya Vibanda Kusudi la sikukuu hizi ilikuwa kumshukuru Mungu na kukumbuka mambo ya ajabu aliyofanya kuwaokoa, kuwalinda na kuwapa watu wake.