22 lines
858 B
Markdown
22 lines
858 B
Markdown
# tia utumwani, katika kifungo
|
|
|
|
## Ufafanuzi
|
|
|
|
"Kutia utumwani" mtu ina maana ya kumlazimisha mtu huyo kumtumikia bwana au nchi tawala. "Kutiwa utumwani" au "kuwa kifungoni" ina maana ya kuwa chini ya utawala wa kitu au mtu.
|
|
|
|
Mtu ambaye yupo katika utumwa au kifungoni anatakiwa kutumikia wengine bila malipo; hayupo huru kufanya anavyotaka.
|
|
|
|
"kutia utumwani" pia ina maana ya kuchukua uhuru wa mtu.
|
|
|
|
Neno lingine la "kifungoni" ni "utumwa".
|
|
|
|
Kwa njia ya tamathali, wanadamu ni "wafungwa" wa dhambi hadi Yesu awaweke huru kutoka katika utwala na nguvu yake.
|
|
|
|
Mtu anapompokea maisha mapya ndani ya Yesu, anasitisha kuwa mtumwa wa dhambi na anakuwa mtumwa wa utakatifu.
|
|
|
|
|
|
Mapendekezo ya Tafsiri
|
|
|
|
Msemo "tia utumwani mwa" au "kuwa kifungoni mwa" unaweza kutafsiriwa kama "kulazimishwa kuwa mtumwa wa" au "kulazimishwa kumtumikia" au "kuwa chini ya utawala wa".
|
|
|