sw_tw/bible/other/enslave.md

858 B

tia utumwani, katika kifungo

Ufafanuzi

"Kutia utumwani" mtu ina maana ya kumlazimisha mtu huyo kumtumikia bwana au nchi tawala. "Kutiwa utumwani" au "kuwa kifungoni" ina maana ya kuwa chini ya utawala wa kitu au mtu.

Mtu ambaye yupo katika utumwa au kifungoni anatakiwa kutumikia wengine bila malipo; hayupo huru kufanya anavyotaka.

"kutia utumwani" pia ina maana ya kuchukua uhuru wa mtu.

Neno lingine la "kifungoni" ni "utumwa".

Kwa njia ya tamathali, wanadamu ni "wafungwa" wa dhambi hadi Yesu awaweke huru kutoka katika utwala na nguvu yake.

Mtu anapompokea maisha mapya ndani ya Yesu, anasitisha kuwa mtumwa wa dhambi na anakuwa mtumwa wa utakatifu.

Mapendekezo ya Tafsiri

Msemo "tia utumwani mwa" au "kuwa kifungoni mwa" unaweza kutafsiriwa kama "kulazimishwa kuwa mtumwa wa" au "kulazimishwa kumtumikia" au "kuwa chini ya utawala wa".