sw_tw/bible/other/devour.md

539 B

meza

Ufafanuzi

Msemo wa "meza" una maana ya kula au kutumia kwa hali ya fujo.

Kutumia neno hili kwa hisi ya tamathali, Paulo anatahadharisha waumini kutojimeza wao kwa wao, akimaanisha kutojishambulia au kuangamizana wao kwa wao kwa maneno au matendo (Wagalitia 5:15).

Pia katika hisi ya tamathali, msemo "kumeza" mara kwa mara hutumika kwa maana ya "kuangamiza kabisa" kama kuzungumzia juu ya mataifa kumeza mengine au moto kumeza majengo na watu.

Msemo huu pia unaweza kutafsiriwa kama "kumeza kabisa" au "kuangamiza kabisa".