sw_tw/bible/names/luke.md

624 B

Luka

Ufafanuzi

Luka alikuwa mwandishi wa vitabu viwili vya Agano Jipya: injili ya Luka na kitabu cha Matendo ya Mitume.

Katika barua yake kwa Wakolosai,Paulo alimtaja Luka kama daktari. Paulo anamtaja Luka kwenye barua zake mbili. Inadhaniwa kuwa Luka alikuwa Mgiriki na Myunani kabla hajamjua Kristo. Katika injili yake, Luka anajumuisha matukio yanayoonesha upendo wa Yesu kwa watu wote, Wayahudi na Wayunani. Luka alifuatana na Paulo katika safari mbili za kimisionari na kumsaidia na kazi zake, Katika maandiko kadhaa ya awali ya kanisa, inasemekana kuwa Luka alizaliwa katika mji wa Antiokia ndani ya Shamu.