sw_tw/bible/names/lot.md

533 B

Lutu

Ufafanuzi

Lutu lilikuwa jina la mpwa wa Abrahamu. Alikuwa mwana wa ndugu yake Abrahamu, Harani. Lutu alisafiri na Abrahamu kwenda nchi ya Kanaani na kuishi katika mji wa Sodoma Lutu alikuwa babu wa Wamoabi na Waamoni. Wafalme maadui walipovamia Sodoma na kumteka Lutu, Abrahamu alikuja na mamia kadha ya wanaume kumuokoa Lutu na kurudisha mali zake. Watu walioishi katika mji wa Sodoma walikuwa watu waovu sana kwa hiyo Mungu aliuangamiza mji huo. Lakini kwanza alimwambia Lutu na familia ya kuuondoka mji ili watoroke.