sw_tw/bible/names/joppa.md

399 B

Yafa

Ufafanuzi

Katika nyakati za Biblia, mji wa Yafa ulikuwa mji muhimu wa kibiashara uliopo Bahari ya Kati, kusini mwa uwanda wa Sharoni.

Eneo la zamani la Yafa ndio mji wa leo wa Yafa, ambayo sasa ni sehemu ya Tel Aviv. Katika Agano la Kale, Yafa ndio mji ambao Yona alipanda boti kwenda Tarshishi. Katika Agano Jipya, mwanamke wa Kikristo aitwaye Tabitha alifia Yafa na Petro alimfufua.