sw_tw/bible/names/johntheapostle.md

564 B

Yohana (mtume)

Ufafanuzi

Yohana alikuwa mmoja wa mitume kumi na mbili na rafiki wa karibu wa Yesu.

Yohana na ndugu yake Yakobo walikuwa wana wa mvuvi wa samaki aitwaye Zebedayo. Katika injili aliyoandika kuhusu maisha ya Yesu, Yohana alijieleza kama "mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda." Hii inaonehsa kuwa Yohana alikuwa rafiki wa karibu wa Yesu. Mtume Yohana aliandika vitabu vitano katika Agano Jipya: injili ya Yohana, Ufuno wa Yesu Kristo, na barua tatu zilionadikwa kwa waumini wengine. Noti kuwa mtume Yohana alikuwa mtu tofauti na Yohana mbatizaji.