sw_tw/bible/names/jezreel.md

610 B

Yezreeli

Ufafanuzi

Yezreeli lilikuwa jina la mji muhimu Israeli katika eneo la kabila la Isakari, lililokuwa kusini magharibi mwa Bahari ya Chumvi.

Mji wa Yezreeli ni moja ya alama za magharibi za uwanda wa Megido, ambayo pia unaitwa "Bonde la Yezreeli." Wafalme kadhaa wa Israeli walikuwa na majumba yao ya utawala katika mji wa Yezreeli. Bustani la mizabibu la Nabothi ilikuwa karibu na nyumba ya mfalme Ahabu ndani ya Yezreeli. Nabii Eliya alitabiri dhidi ya Ahabu huko. Mke muovu wa Ahabu, Yezebeli, aliuwawa Yezreeli. Matukio mengine ya muhimu yalitokea katika mji huu, yakiwemo mapigano kadhaa.