sw_tw/bible/names/jehu.md

719 B

Yehu

Ufafanuzi

Yehu lilikuwa jina la wanaume wawili katika Agano la Kale.

Yehu mwana wa Hanani alikuwa nabii wakati wa utawala wa Mfalme Ahabu na Mfalme Yehoshafati wa Yuda. Yehu mwana (uzao) wa Yehoshafati alikuwa jemedari katika jeshi la Israeli ambaye alitiwa mafuta kuwa mfalme kwa amri ya nabii Elisha. Yehu aliua vitu viwili viovu: Mfalme Yoramu wa Israeli na Mfalme Ahazia wa Yuda. Mfalme Yehu pia aliwaua ndugu wote wa mfalme wa zamani Ahabu, na akafanya yule malkia muovu Yezebeli auwawe. Yehu aliaangamiza sehemu zote za kumuabudia Baali ndani ya Samaria na kuwaua manabii wote wa Baali. Mfalme Yehu alimtumikia Mungu mmoja wa kweli, Yahwe, na alikuwa mfalme juu ya Israeli kwa miaka ishiri na nane.