sw_tw/bible/names/jehoram.md

849 B

Yehoramu, Yoramu

Ufafanuzi

Yehoramu lilikuwa jina la wafalme wawili tofauti katika Agano la Kale. Wafalme wote hao wawili walijulikana kama "Yoramu."

Mfalme mmoja Yehoramu alitawala ufalme wa Yuda kwa miaka minane. Alikuwa mwana wa Mfalme Yehoshafati. Huyu ndiye mfalme anayejulikna zaidi kama Yoramu. Mfalme Yehoramu mwingine alitawala ufalme wa Israeli kwa miaka kumi na mbili. Alikuwa mwana wa Mfalme Ahabu. Mfalme Yehoramu wa Yuda alitawala wakati wa manabii Yeremia, Danieli, Obadia, na Ezekieli wakitabiri katika ufalme wa Yuda. Yehoramu pia alitawala kwa muda kiasi wakati baba yake Yehoshafati alipokuwa akitawala Yuda. Tafsiri zingine zinaweza kuchagua kutumia jina "Yehoramu" pale ambapo huyu mfalme wa Israeli anatajwa na "Yoramu" kwa mfalme wa Yuda. Njia nyingine ya kumtambua vizuri kila mmoja ni kuongeza jina la baba yake.