sw_tw/bible/names/jehoiakim.md

558 B

Yehoyakimu

Ufafanuzi

Yehoyakimu alikuwa mfalme muovu aliyetawala ufalme wa Yuda, kuanzia mwaka 608 K.K. Alikuwa mwana wa mfalme Yosia. jina lake mwanzoni lilikuwa Eliakimu.

Farao wa Misri Neko alibadili jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu na kumfanya kuwa mfalme wa Yuda. Neko alimlazimisha Yehoyakimu kulipa kodi ya juu kwa Misri. Yuda ilipovamiwa baadaye na mfalme Nebukadreza, Yehoyakimu alikuwa miongoni mwao wale walikamatwa na kupelekwa Babeli. Yehoyakimu alikuwa mfalme mwovu aliyeingoza Yuda mbali na Yahwe. Nabii Yeremia alitabiri dhidi yake.