sw_tw/bible/names/jehoiada.md

555 B

Yehoyada

Ufafanuzi

Yehoyada alikuwa kuhani aliyemsaidia kumficha na kumlinda mwana wa mfalme Ahazia, Yoashi hadi alipofikisha umri wa kuweza kutangazwa kuwa mfalme.

Yehoyada alimpangia mamia ya walinzi kumlinda Yoashi alipokuwa mdogo wakati akitangazwa kuwa mfalmena watu hekaluni. Yehoyada aliwaongoza watu kuondoa madhabahu yote ya mungu wa uongo Baali. Maisha yake yote yaliyosalia, kuhani Yehoyada alimshauri mfalme Yoashi kwa kumsaidia kumtii Mungu na kuwatawala watu kwa hekima. Mwanamme mwingine aliyeitwa Yehoyada alikuwa baba wa Benaya.