sw_tw/bible/names/hittite.md

744 B

Mhiti

Ufafanuzi

Wahiti walikuwa ni uzao wa Hamu kupitia kwa mtoto wake Kanaani. Walifanyika kuwa dola kubwa katika eneo ambalo kwa sasa linaitwa Uturuki na Kaskazini mwa Palestina. Ibrahimu alinunua sehemu ya ardhi kutoka kwa Efroni, Mhiti ili aweze kumzika Sara katika pango huko. Hatimaye, Ibrahimu na wazao wake kadhaa walizikwa katika pango hilo pia. Wazazi wa Esau walihuzunika sana baada ya Esau kuoa wanawake Wahiti. Mmoja kati ya watu wa Daudi aliyekuwa na nguvu aliitwa Uria Mhiti. Miongoni mwa wanawake aliowaoa Sulemani walikuwa ni Wahiti. Wanawake hawa wa kigeni waliugeuza moyo wa Sulemani kutoka kwa Mungu kwasababu ya miungu waliyoiabudu. Wahiti walikuwa mara zote ni hofu kwa waisraeli, kimwili na kiroho pia.