sw_tw/bible/names/hilkiah.md

508 B

Hilikia

Ufafanuzi

Hilikia lilikuwa ni jina la kuhani mkuu katika kipindi cha utawala wa mfalme Yosia. Hilikia alipata kitabu cha sheria, katika kipindi ambacho hekalu lilifanyiwa matengenezo na akamuru kitabu hicho kipelekwe kwa mfalme Yosia. Baada ya kusomewa kitabu cha sheria, Yosia alihuzunika na aliwafanya watu wa Israeli kumwabudu Yahweh tena na kutii sheria zake. Mtu mwingine aliyeitwa Hilikia alikuwa ni mwana wa Eliyakimu na alifanya kazi ikulu kipindi cha utawala wa mfalme Hezekia.