sw_tw/bible/names/geshur.md

424 B

Geshuri

Ufafanuzi

Katika kipindi cha Mfalme Daudi, Geshuri ilikuwa ufalme mdogo uliokuwa upande wa mashariki wa Ziwa la Galilaya, kati ya nchi za Israeli na Aramu.

Mfalme Daudi alimuoa Maaka, binti wa mfalme wa Geshuri na akamzalia mwana wa kiume, Absalomu.

Baada ya kumuua ndugu yake Amnoni, Absalomu alikimbilia kaskazini mashariki mwa Yerusalemu hadi Geshuri, umbali wa kama maili 88. Alikaa kule miaka mitatu.