sw_tw/bible/names/esther.md

673 B

Esta

Ufafanuzi

Esta alikuwa mwanamke wa Kiyahudi ambaye alikuwa malkia wa ufalme wa Ashuri katika kipindi cha mateka ya Babeli kwa Wayahudi.

Kitabu cha Esta kinaelezea simulizi ya jinsi Esta alivyokuwa mke wa mfalme wa Waashuri Ahasuero na jinsi Mungu alivyomtumia kukomboa watu wake.

Esta alikuwa yatima ambaye alikuzwa na binamu yake mkubwa, Mordekai.

Kutii kwake kwa baba yake wa kambo kulimsaidia kuwa mtiifu kwa Mungu.

Esta alimtii Mungu na kuweka maisha yake hatarini ili kuwakomboa watu wake, Wayahudi.

Simulizi ya Esta inaelezea utawala wa Mungu wa enzi juu ya matukio na historia, haswa jinsi anavyolinda watu wake na kutumika kupitia wale wanaomtii.