sw_tw/bible/names/baasha.md

557 B

Baasha

Ufafanuzi

Baasha alikuwa miongoni mwa wafalme waovu wa Israeli,waliowashawishi Waisraeli kuabudu vinyago.

  • Baasha alikuwa mfalme wa tatu wa Israeli na alimiliki kwa miaka ishirini na minne, wakati Asa akiwa mfalme wa Yuda.
  • Alikuwa jemedari wa jeshi aliyejifanya mfalme baada ya kumwua mfalme Nadabu, mtangulizi wake.
  • Kulikuwa na mapigano mengi wakati wa utawala wa Baasha kati ya ufalme wa Israeli na Yuda, hasa na Asa mfalme wa Yuda.
  • Dhambi nyingi alizozitenda Baasha hatimaye zilimfanya Mungu kumwondoa katika nafasi yake kwa kifo.