sw_tw/bible/kt/kingofthejews.md

628 B

Mfalme wa Wayahudi

Ufafanuzi

Usemi, "Mfalme wa Wayahudi" ni jina linalomaanisha Yesu, Masihi.

Mara ya kwanza Biblia inaandika hili jina wakati linapotumika na wanaume wenye hekima waliosafiri kwenda Bethlehemu wakimtafuta mtoto aliye "Mfalme wa Wayahudi." Malaika alimfunulia Mariamu kuwa mwanaye, mzawa wa mfalme Daudi, atakuwa mfalme ambaye ufalme wake utadumu milele. Kabla Yesu hajasulibishwa, askari Wakirumi walimdhihaki Yesu kwa kumuita "Mfalme wa Wayahudi." JIna hili liliandikwa pia katika kipande cha mbao na kupigwa msumari juu ya msalaba wa Yesu. Yesu kweli ni Mfalme wa Wayahudi na mfalme wa viumbe vyote.