sw_tw/bible/kt/iniquity.md

455 B

uovu

Ufafanuzi

Neno "uovu" ni neno ambalo liko karibu kwa maana na neno "dhambi," lakini inaweza kumaanisha zaidi matendo ya ufahamu mabaya au uovu mkubwa.

Neno "uovu" ina maana halisi ya kupindisha au kupotosha (sheria). Inamaanisha udhalimu mkubwa. Uovu unaweza kuelezwa kama matendo ya kudhuru ya makusudi dhidi ya watu wengine. Maana zingine za uovu ni pamoja na "ukaidi" na "kunyima," ambayo yote ni maneno yanayoeleza hali za dhambi mbaya.