sw_tw/bible/kt/heart.md

1.2 KiB

Moyo

Ufafanuzi

Katika Biblia, neno 'moyo' limetumika mara nyingi kimfano kurejelea mawazo ya mtu, hisia, tamaa au utashi. Kuwa na 'moyo mgumu' ni msemo wa kawaida wenye maana ya mtu anayemwasi Mungu kwa ukaidi. Msemo "kwa moyo wote'' au '' kwa moyo wangu wote'' una maana ya kufanya kitu kwa kujitoa kikamilifu na kwa uhiari. Msemo mwingine '' weka moyoni" una maana kuchukulia kitu kwa umakini na kukitumia katika maisha. Maneno " kuvunjika moyo'' humwelezea mtu ambaye ana huzuni. Wamekuwa wameumizwa kihisia za ndani

Mapendekezo ya tafsiri Baadhi ya lugha hutumia sehemu tofauti za mwili kama vile 'tumbo' au 'ini' kurejelea mawazo haya. Lugha zingine zaweza kutumia neno moja kuelezea dhana hizi na neno jingine kueleza dhana zingine. kama 'moyo' au sehemu nyingine ya mwili haina maana hii, lugha zingine zaweza kuhitaji kutumia maneno ya moja kwa moja kama vile 'fikra' au 'hisia' au 'tamaa.' Kwa kutegemeana na muktadha, maneno "kwa moyo wangu wote" yaweza kutafsiriwa kama "kwa nguvu zangu zote" au "kwa kujitoa kimamilfu" Maneno kama "weka moyoni" yaweza kutafsiriwa kama 'shughulikia kwa umakini' au fikiria kwa uangalifu" "kuvunjika moyo" ina maana ya kuwa 'mwenye huzuni' au 'kujisikia kuumizwa kwa ndani"