sw_tw/bible/kt/glory.md

698 B

utukufu, fahari

Ufafanuzi

Kwa ujumla, msemo "utukufu" una maana ya heshima, fahari, na ukuu wa hali ya juu sana. Kitu chochote ambacho kina utukufu kinasemekana kuwa na "fahari".

Mara nyingi, "utukufu" ina maana ya kitu chenye thamani kubwa na umuhimu. Katika muktadha zingine inawasilisha ufahari, mwanga, au hukumu.

Kwa mfano, msemo "utukufu wa wafugaji" una maana ya malisho yaliyostawi sana ambapo kondoo wao walikuwa na nyasi nyingi za kula.

Utukufu haswa hutumika kumfafanua Mungu, ambay ana ufahari zaidi ya yeyote au chochote katika ulimwengu. Kila kitu katika tabia yake huonyesha utukufu na ufahari wake.

Msemo "kutukuzwa na" una maana ya kujidai juu ya au kujivunia na kitu.