sw_tw/bible/kt/exalt.md

899 B

tukuza, kutukuza

Ufafanuzi

Kutukuza ni kusifu kwa juu sana na kumheshimu mtu. Inaweza kumaanisha kumweka mtu katika nafasi ya juu.

Katika Biblia, msemo "tukuza" unatumika sana kwa ajili ya kumtukuza Mungu.

Mtu anapojitukuza mwenyewe, ina maana anawaza juu yake mwenyewe kwa hali ya kujiinua au namna ya kiburi.

Mapendekezo ya Tafsiri

Njia za kutafsiri "tukuza" zinaweza kujumuisha "kusifu kwa juu" au "kuheshimu sana" au "sifu sana" au "kuzungumza kwa juu sana"

Katika baadhi ya muktadha, inaweza kutafsiriwa kwa neno au msemo ambao una maana ya "kuweka nafasi ya juu zaidi" au "kutoa heshima zaidi" au "kuzungumza kuhusu kwa kiburi".

"Usijitukuze mwenyewe" inaweza kutafsiriwa kama "Usijiwazie kuwa juu sana" au "Usijidai juu yako mwenyewe".

"Wale wanaojiinua wenyewe" inaweza kutafsiriwa kama "Wale ambao hufikiri kwa kiburi kuhusu wao wenyewe" au "Wale wanaojidai juu yao wenyewe"