sw_tw/bible/kt/disciple.md

1.1 KiB

mfuasi

Ufafanuzi

Msemo wa "mfuasi" una maana ya mtu anayetumia muda mwingi na mwalimu, akijifunza kutoka kwa tabia na mafunzo ya mwalimu huyo.

Watu waliomfuata Yesu, wakimsikiliza mafundisho yake na kuyatii, walijulikana kama "wanafunzi" wake.

Yohana Mbatizaji pia alikuwa na wanafunzi.

Katika kipindi cha huduma ya Yesu, kulikuwa na wanafunzi wengi waliomfuata na kusikiliza mafunzo yake.

Yesu alichagua watume kumi na wawili wawe wafuasi wake wa karibu; wanamume hawa wakaja kujulikana kama "mitume" wake.

Watume kumi na wawili waliendelea kujulikana kama "wanafunzi" wake au "wale kumi na wawili".

Kabla tu ya Yesu kwenda juu mbinguni, aliwaamuru wanafunzi wake kuwafundisha watu wengine juu ya kuwa wafuasi wa Yesu pia.

Yeyote anayemwamini Yesu na kumtii mafunzo yake anaitwa mfuasi wa Yesu.

Mapendekezo ya Tafsiri

Msemo "mwanafunzi" unaweza kutafsiriwa kwa neno au msemo wenye maana ya "mfuasi" au "mwanafunzi".

Hakikisha ya kwamba tafsiri ya msemo huu haimaanishi mwanafunzi anayejifunza darasani.

Tafsiri ya msemo huu unatakiwa kuwa tofauti na tafsiri ya "mtume".