sw_tw/bible/kt/covenant.md

703 B

Agano

Ufafanuzi

Agano ni makubaliano kati ya pande mbili kuwa upande mmoja au zote unapaswa kutekeleza.

  • Makubaliano haya yanaweza kuwa ya mmoja mmoja, kati ya makundi ya watu au kati ya Mungu na watu.
  • Watu wanapoweka agano kati yao wanaahidi kufanya jambpo fulani ambalo wanapaswa wafanye.
  • Mfano wa maagano ya wanadamu ni maagano ya ndoa, makubaliano ya biashara na mikataba kati ya nchi.
  • Katika Biblia Mungu ameweka maagano mbalimbali na watu wake.
  • Katika baadhi ya maagano Mungu aliahidi kutekeleza bila masharti yoyote. Kwa mfano Mungu alipoweka agano na mwanadamu kuwa hataiangamiza duinia kwa mafuriko.
  • Katika maagano mengine Mungu ameahidi kutekeleza kama watu watamtii yeye.