1.1 KiB
1.1 KiB
damu
Ufafanuzi
Neno "damu" linamaanisha kimiminika chekundu kinachotoka katika ngozi ya mtu panapokuwa na jeraha au kidonda. Damu inaleta viini lishe vya uhai katika mwili wote wa mtu.
- Damu inaashiria uhai na inapomwagwa, inaashiria kifo.
- Watu walipotoa sadaka kwa Mungu, walimwua mnyama na kumimina damu yake juu ya madhabahu. Hii inaashiria kutolewa kwa uhai wa mnyama kulipa dhambi za watu.
- Kupitia kifo chake msalabani, Damu ya Yesu hutakasa watu kutokana na dhambi zao na kulipa kwa ajili ya adhabu wanayostahili kwa ajili ya dhambi zao.
- Kifungu "mwili na damu" kinarejerea wanadamu.
- Kifungu "mwili wake na damu yake" inarejerea kwa watu wanaohusiana kibaolojia.
Maoni ya Kutafasiri
- Neno hili litumika kwa kulingana na neno lifaalo katika lugha lengwa.
- Kielezi "mwili na damu" chaweza kutafasiriwa kama "watu" au "wanadamu".
- Kwa kutegemea mazingira, kifungu "mwili wangu na damu yangu mwenyewe" yaweza kutafasiriwa kama "familia yangu" au "ndugu zangu" au "watu wangu."
- Ikiwa kuna kionyeshi katika lugha lengwa kinachotumika kwa maana hii, kifungu hicho kitumike kutafasiri "mwili na damu"