sw_tw/bible/other/lordgod.md

1.0 KiB

Bwana

Ufafanuzi

Neno "Bwana" linamaanisha mtu anayemiliki na mwenye mamlaka juu ya watu wengine. Inapokuwa na herufi kubwa, ni jina linalomaanisha Mungu. (Noti hata hivyo inapotumika kama njia ya kumtambua mtu mwanzo mwa sentesi inaweza kuwa na herufi kubwa na kuwa na maana ya "mkuu.")

Katika Agano la Kale, msemo huu pia unatumika maneno kama, "Bwana Mungu Mkuu" au "Bwana Yahwe" au "Yahwe Bwana wetu." Katika Agano Jipya, mitume walitumia neno hili katika misemo kama, "Bwana Yesu" na "Bwana Yesu Kristo," illiyoonyesha kuwa Yesu ni Mungu. Neno "Bwana" katika Agano Jipya pia linatumika peke yake kama njia ya moja kwa moja ya kumtambua Mungu, hasa katika nukuu za kutoka Agano la Kale. Kwa mfano, maandishi ya Agano la Kale ya, "Amebarikiwa ajaye kwa jina la Yahwe" na Agano Jipya lina, "Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana." Katika ULB na UDB, jina "Bwana" linatumika tu kutafsiri maneno halisi ya Kihebrania na Kigriki yanayomaanisha "Bwana." Halitumiki kama tafsiri ya jina la Mungu (Yahwe), kama inavyofanywa na tafsiri zingine.