sw_tw/bible/other/leprosy.md

761 B

ukoma, mkoma

Ufafanuzi

Neno "ukoma" linatumika katika Biblia kumaanisha aina kadhaaza magonjwa ya ngozi. "Mkoma" ni mtu mwenye ukoma. Neno "ukoma" pia linaweza kutumika kuelezea mtu au sehemu ya mwili iliyoadhirika na ukoma.

Aina flani za ukoma zinasababisha ngozi kupoteza rangi na mabaka meupe, kama Miriamu na Naamani walivyokuwa na ukoma. Katika nyakati za sasa, ukoma mara nyingi husababisha mikono, miguu, na sehemu zingine za mwili kuharibika. Kulingana na maelekezo ambayo Mungu aliwapa Waisraeli, mtu akiwa na ukoma, alionekana "mchafu" na ilimbidi kukaa mbali na watu wengine ili asiwaambukize na ugonjwa. Mkoma kawaida angasema "mchafu" ili wengine waonywe wasije karibu yake. Yesu aliponya wakoma wengi, pamoja na aina zingine za magonjwa.