sw_tw/bible/other/lawful.md

930 B

halali, ipasavyo, kinyume na sheria

Ufafanuzi

Msemo "halali" unamaanisha kitu kinachoruhusiwa kufanywa kulingana na sheria au mahitaji mengine. Kinyume cha hiki ni "kinyume na sheria" inyomaanisha "sio halali."

Katika Biblia, kama kitu kinasemwa kuwa "halali" inamaanisha inaruhusiwa na sheria ya kimaadili ya Mungu, au kwa sheria ya Musa au sheria zingine za Kiyahudi. Kitu ambacho "sio halali" "hakiruhusiwi" na sheria hizo. Kufanya kitu "ipasavyo" inamaanisha kuifanya "sawa" au "katika njia sahihi." Mambo mengi Wayahudi waliyoona ni halali au sio halali hayakuwa kwenye makubaliano na sheria za Mungu kuhusu kuwapenda wengine. Kulinga na mazingira, njia za kuafsiri "halali" ni pamoja na, "kuruhusu" au "kulingana na sheria ya Mungu" au "kufuatana na sheria zetu" au "sawa" au inafaa." Msemo "Je ni halali" inaweza pia kutafsiriwa kama "Je, sheria zetu zinaruhusu" au "Hilo ni jambo ambalo sheria zetu zinaruhusu?"