sw_tw/bible/other/inquire.md

817 B

ulizia

Ufafanuzi

Usemi "ulizia" inamaana kumuomba mtu taarifa. Usemi wa "kuulizia kwa"mara nyingi unatumika kumaanisha kumuomba Mungu hekima au msaada.

Agano la kale limetunza kumbukumbu ya mifano kadhaa ambapo watu walimuuliza Mungu. Neno pia linaweza kutumika kwa mfalme au afisa wa serikalini kufanya utafiti katika kumbukumbu za maandishi rasmi. Kulingana na mazingira, "ulizia" inaweza kutafsiriwa kama "kuomba" au "kuomba taarifa." Usemi "kumuuliza Yahwe" inaewza kutafsiriwa kama "kumuomba Yahwe uongozo" au "kumuuliza Yahwe nini cha kufanya." "Kuulizia juu ya" kitu inaweza kutafsiriwa ka "kuuliza maswali kuhusu" au "kuulizia taarifa kuhusu." Yahwe anaposema, "Sitaulizwa na wewe" hii inaweza kutafsiriwa kama, "Sita kuruhusu wewe uniombe taarifa" au "hautaruhusiwa kutafuta msaada kutoka kwangu."