sw_tw/bible/other/highplaces.md

1.0 KiB

Sehemu za juu

Ufafanuzi

Maneno 'sehemu za juu' yanarejelea madhabahu na maeneo matakatifu yaliyokuwa yakitumika katika kuabudu miungu. Mara zote maeneo haya yalikuwa sehemu za juu kama vile milimani au sehemu za vilima. Wafalme wengi wa Israeli walitenda dhambi kinyume na Mungu kwa kujenga madhabahu kwa ajili ya miungu katika sehemu hizi za juu. Hii iliwafanya watu kujishughulisha kwa undani katika ibada ya miungu. Wakati mfalme aliyemcha Mungu, alipoanza kutawala juu ya Yuda au Israeli, mara kwa mara waliweza kuonda sehemu hizi za juu na madhabahu ili kuzuia ibada za hizi miungu. Hata hivyo, baadhi ya wafalme wazuri hawakuwa makini sana na hawakuziondoa sehemu hizi za juu, na matokeo yake taifa lote la Israeli liliendelea kuabudu miungu.

Mapendekezo ya tafsiri Namna nyingine ya kutafsiri maneno haya twaweza kusema, " maeneo/sehemu iliyoinuliwa kwa ajili ya ibada ya miungu' au 'kilele cha mlima cha ibada ya miungu.' Hakikisha kuwa maneno unayoyatumia yawe na maana ya madhabahu ya miungu na siyo tu maeneo ya juu zilipo madhabahu hizo.