sw_tw/bible/other/heir.md

465 B

Mrithi

Ufafanuzi

Mrithi ni mtu ambaye kisheria hupoke mali au pesa za mtu aliyekufa. Katika nyakati za Biblia, mrithi mkuu alikuwa ni mtoto wa kwanza ambaye alipokea sehemu kubwa ya mali au pesa za baba yake. Biblia hutumia neno mrithi kama lugha ya picha kumaanisha Wakristo wanapopokea baraka za kiroho kutoka kwa Mungu, baba yao wa kiroho. Kama watoto wa Mungu, Wakristo ni warithi pamoja na Yesu Kristo. Hii inaweza kutafsiriwa kama "warithi wenza.'