sw_tw/bible/other/heal.md

916 B

Ponya, tibu

Ufafanuzi

Maneno 'ponya' na 'tibu' yote mawili yana maana ya kumfanya mtu aliye mgonjwa, aliyejeruhika na asiyejiweza (mlemavu) kuwa na afya nzuri tena. Mtu aliyeponya au kutibiwa amekuwa amefanywa mzima na mwenye afya nzuri tena. Uponyaji waweza kutokea tu kiuasilia bila kutumia kitu chochote, hii ni kwasababu Mungu alitupa miili yenye uwezo wa kupona na kurudia hali yake ya kawaida hata kama ina vidonda au magonjwa ya aina mbalimbali. Aina hii ya uponyaji hutokea polepole. Hata hivyo hali zingine kama kuwa upofu au ulemavu, na magonjwa mengine kama ukoma hayawezi kupona menyewe tu. Wakati watu wenye magonjwa kama haya wanapoponywa huwa ni muujiza ambao hautokei mara kwa mara. Kwa mfano, Yesu aliponya watu wengi walikuwa vipofu, vilema na wagonjwa na wakapona hapo hapo. Mitume pia waliponya watu kwa miujiza, kwa mfano Petro alimfanya mlevu aweze kutembea mara hiyo.