sw_tw/bible/other/head.md

1.9 KiB

Kichwa

Ufafanuzi

Katika Biblia neno 'kichwa' lilmetumika kama tamathali ya semi likiwa lina maana nyingi: Mara nyingi neno hili limetumika kurejelea hali ya kuwa na mamlaka juu ya watu , kwa mfano, "mmenifanya kichwa cha mataifa" Sentensi hiyo yaweza kutafsiriwa kuwa "mmenifanya kuwa mtawala" au "mmenipa mamlaka juu ya..." Yesu anaitwa 'kichwa cha kanisa.' Kama ambavyo kichwa cha mtu huongoza viungo vingine vya mwili, hivyo na Yesu huongoza na huelekeza viungo vingine vya mwili wake, yaani kanisa. Agano la Jipya linatufundisha kuwa mme ni "kichwa'' au mwenye mamlaka kwa mkewe. Amepewa wajibu wa kumwongoza na kumwelekeza mkewe na familia. Maneno yanayosema "wembe hautagusa kich chake" maana yake ni kwamba" hatakata au hatanyoa nywele zake. Neno 'kichwa' laweza pia kurejelea mwanzo au asili ya kitu fulani, mfano 'kichwa cha mtaa" Maneno kama "kichwa cha nafaka" hurejelea sehemu ya juu ya ngano au mche wa shayiri ambao una mbegu ndani yake. Mfano mwingine wa 'kichwa' ni pale unapotumika kuwakilisha mtu mzima. Mfano, 'kichwa cheupe' humrejelea mtu mzee au tunaposema ' kicha cha Yusufu, tunamaanisha Yusufu mwenyewe. Msemo unaosema 'acha damu yao iwe juu ya kichwa chake' humaanisha kuwa mtu yule anawajibika kwa vifo vyao na atapokea adhabu/hukumu yake.

Mapendekezo ya tafsiri Neno 'kichwa' laweza kutafsiriwa kama 'mamlaka' au 'mtu anayeongoza na kuelekeza' au 'mtu anayewajibika kwa..' kwa kutegemea na muktadha wenyewe. Maneno kama ' kichwa cha' hurejelea mtu mwenyewe mzima, na hivyo maneno hayo yaweza kutafsiriwa kwa kutumia jina la mtu husika. kwa mfano ''kichwa cha Yusufu'' ina maana ya 'Yusufu' Maelezo kama ' itakuwa juu ya kichwa chake' yanaweza kutafsiriwa kama " itakuwa juu yake'' au 'ataadhibiw'a kwa ajili ya' au 'atawajibika kwa ajili ya... Kwa kutegemea na muktadha wenyewe, maana zingine za neno kichwa zaweza kuwa "mwanzo' au "asili'' au ''chanzo'' au "mtawala" au ''juu ya''