sw_tw/bible/other/haughty.md

711 B

Kiburi

Ufafanuzi

Neno 'Kiburi' lina maana ya kuwa mwenye kujisifu, kujigamba au kujiona. Inarejelea mtu ambaye hujiona mwenyewe kuwa ni wa juu sana kuliko wengine. Mara nyingi neno hili humzungumzia majivuno ya mtu ambaye huendelea kufanya dhambi kinyume na Mungu. Mara kwa mara mtu mwenye kiburi hujivuna na kujiinua yeye mwenyewe Mtu mwenye kiburi ni mpambavu, hana hekima. Neno 'kiburi' laweza kutafsiriwa kama 'majivuno' ' majigambo' 'kujiinua' au kujiona. Maneno "macho ya kiburi'' ni Lugha ya picha ambayo yaweza kutafsiriwa kama "kuangalia kwa kiburi'' au " kuwaangalia wengine kama watu wasio na umuhimu'' au ''mtu mwenye kiburi anayewadharau wengine kwa kuwaona kuwa wako chini.''