sw_tw/bible/other/hail.md

593 B

Mvua ya mawe

Ufafanuzi

Mvua ya mawe ni vipande vidogo vidogo au vikubwa vya maji yaliyoganda ambayo hushuka kutoka mawinguni. Mawe ya Mvua hushuka kutoka mawinguni katika umbo la kama mpira au vipande vya barafu. Mawe haya ya mvua mara nyingi huwa ni madogo madogo, lakini wakati mwingine yanaweza kuwa makubwa yenye upana wa sentimita 20 hivi na uzito wa kilogramu moja hivi. Kitabu cha Ufunuo katika Agano la Jipya kinazungumzia juu ya mawe ya mvua makubwa yenye uzito wa kilogramu 50 hivi ambayo Mungu atayashusha juu ya dunia ili kuhukumu watu waovu katika siku za mwisho.