sw_tw/bible/other/grape.md

778 B

Zabibu

Ufafanuzi

Mzabibu ni tunda dogo, la duara, laini ambalo huota katika vishada vya mizabibu. Juisi ya mizabibu hutumika kutengeneza divai.

Kuna aina tofauti ya rangi ya mizabibu, kama vile kijani iliyoiva, zambarau au nyekundu.

Mizabibu binafsi inaweza kuwa na ukubwa kama sentimita moja au tatu.

Watu huotesha mizabibu katika bustani inayoitwa mashamba ya mizabibu. Hii huwa mistari mirefu ya zabibu.

Mizabibu ilikuwa chakula muhimu sana wakati wa Biblia na kuwa na mashamba ya zabibu ilikuwa ishara ya utajiri.

Ili kukaa na mizabibu isioze, watu mara kwa mara waliikausha. Mizabibu ya kukaushwa iliitwa "zabibu kavu" na ilitumika kutengeneza keki za zabibu kavu.

Yesu alitoa fumbo juu ya shamba la zabibu kuwafundisha wanafunzi wake juu ya ufalme wa Mungu.