sw_tw/bible/other/gold.md

1020 B

dhahabu

Ufafanuzi

Dhahabu ni chuma cha manjano, cha ubora wa juu sana kinachotumika kutengeneza vito na vyombo vya dini. Ilikuwa chuma ya thamani zaidi katika kipindi cha zamani.

Katika kipindi cha Biblia, aina nyingi tofauti ya vyombo vilitengezwa kwa dhahabu ngumu au kufunikwa na safu nyembamba ya dhahabu.

Vyombo hivi vilijumuisha heleni na vito vingine, sanamu, madhabahu, na vyombo vingine vilivyotumika katika tabenakulo au hekalu, kama vile sanduku la agano.

Katika Agano la Kale, dhahabu ilitumika kama njia ya kubadilishana katika kununua na kuuza. Ilipimwa juu ya mizani kupata thamani yake.

Baadaye, dhahabu na vyuma vingine kama vile fedha vilitumika kutengeneza sarafu kutumiwa kununua na kuuza.

Pale inapomaanisha kitu ambacho sio dhahabu ngumu, lakini ina safu nyembamba tu ya dhahabu, msemo "ya dhahabu" au "kufunikwa kwa dhahabu" inaweza kutumika.

Mara nyingi chombo kinaelezewa kama "rangi ya dhahabu" ambayo ina maana ina rangi ya njano ya dhahabu, lakini haijatengenezwa kwa dhahabu.