sw_tw/bible/other/generation.md

1.1 KiB

kizazi

Ufafanuzi

Msemo "kizazi" una maana ya kundi la watu ambao wote wamezaliwa katika kipindi cha kufanana.

Kizazi pia kinaweza kumaanisha kipindi cha muda. Katika kipindi cha Biblia, kizazi kilichukuliwa kuwa kama miaka 40.

Wazazi na watoto waoo wanatoka katika vizazi viwili tofauti.

Katika Biblia, msemo "kizazi" pia hutumika kitamathali kumaanisha kwa ujumla watu ambao huwa na tabia za kufanana.

Mapendekezo ya Tafsiri

Msemo " kizazi hiki" au "watu wa kizazi hiki" unaweza kutafsiriwa kama "watu wanaoishi sasa" au "nyie watu".

"Kizazi hiki kiovu" inaweza kutafsiriwa kama "watu hawa waovu wanaoishi sasa".

Msemo "kutoka kizazi hadi kizazi" au "kutoka kizazi kimoja hadi kingine" inaweza kutafsiriwa kama "watu wanaoishi sasa, pamoja na watoto na wajukuu wao" au "watu katika kipini chote" au "watu wa kipindi hili na vipindi vya baadaye" au "watu wote na uzao wao".

"Kizazi kinachokuja kitamtumikia; watawaambia kizazi kifuatacho juu ya Yahwe" inaweza kutafsiriwa kama "Watu wengi hapo baadaye watamtumikia Yahwe na kuwaambia watoto na wajukuu wao juu yangu".