sw_tw/bible/other/foreigner.md

714 B

mgeni, ugeni, mgeni

Ufafanuzi

Msemo, "mgeni" una maana ya mtu anayeishi katika nchi ambayo sio yake.

Katika Agano la Kale, msemo huu haswa humaanisha mtu yeyote ambaye alikuja kutoka kwa kundi tofauti la watu na watu ambao anaishi miongoni mwao.

Mgeni pia ni mtu ambaye lugha yake na utamaduni ni tofauti na ya kwako.

Kwa mfano, Naomi na familia yake alipohama kwenda Moabu, walikuwa wageni kule. Naomi na mkwe wake Ruthu walipohamia Israeli baadaye, Ruthu aliitwa "mgeni" kule kwa saba hakuwa wa Israeli kiasili.

Mtume Paulo aliwaambia Waefeso ya kuwa kabla hawajamjua Kristo, walikuwa "wageni" kwa agano la Mungu.

Mara nyingi, "mgeni" hutafsiriwa kama "mgeni" mtu ambaye hajulikani au hajazoeleka.