sw_tw/bible/other/flood.md

1.2 KiB

mafuriko

Ufafanuzi

Msemo "mafuriko" ina maana ya kiasi kikubwa cha maji ambacho kinafunika juu ya nchi.

Msemo huu pia hutumika kitamathali kumaanisha kiasi kikubwa cha kitu, haswa kitu ambacho hutokea ghafla.

Katika kipindi cha Nuhu, watu walikuwa waovu hadi Mungu akasababisha mafuriko duniani kote kuwa juu ya uso wote wa dunia, hata kufunika juu za milima. Kila mtu ambaye hakuwa katika mtumbwi pamoja na Nuhu alizama. Mafuriko yote mengine hufunika eneo dogo la nchi.

Msemo huu pia unaweza kuwa tendo kama, "nchi ilifurika na maji ya mto".

Mapendekezo ya Tafsiri

Njia za kutafsiri maana halisi ya "mafuriko" inaweza kujumuisha, "maji yanayomwagikia" au "kiasi kikubwa cha maji"

Mlinganisho wa kitamathali, "kama mafuriko" unaweza kukaa na msemo halisi, au msemo mbadala unaweza kutumika ambao una maana ya kitu ambacho kina hali ya kutiririka kwake, kama vile mto.

Kwa msemo "kama mafuriko ya maji" pale ambapo maji yametajwa tayari, neno "mafuriko" linaweza kutafsiriwa kama "kiasi kikubwa sana" au "yanayomwagikia".

Msemo huu unaweza kutumika kama sitiari kama, "usiruhusu mafuriko kunizoa juu yangu", ambayo ina maana ya "usiruhusu maafa haya makubwa kutokea kwangu" au "usiniache niteketezwe kwa maafa" au "usiache hasira yako initeketeze".